Mkuu wa Mkoa
wa Rukwa kamishna Mstaafu Zelote Stephen ametembelea magereza mawili ya mkoa
huo ili kusikiliza vilio vya wafungwa na kutafuta utaratibu wa kuweza
kuwasaidia na kuondoa msongamano katika magereza hayo.
 |
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen akielekezwa na maafisa wa magereza mifugo inayomilikiwa na jeshi hilo katika gereza la Mollo. |
Mkuu wa Mkoa
aliyeambatana na wawakilishi wawili wa Mahakama kuu pamoja na kamati ya ulinzi
na usalama ya mkoa kabla ya kuongea na wafungwa na mahabusu aliweza kuangalia
miundo mbinu ya magereza hayo ikiwemo sehemu za kulalia, kupikia, vyoo
wanavyotumiapamoja na huduma ya maji na umeme ili kujua ubora na uimara wa
miundombinu hiyo.
Mkuu wa Mkoa
ili kujiridhisha na huduma ya chakula katika gereza hilo aliomba bakuli la
ugali pamoja na maharage na kuanza kula mbele ya wafungwa hao, jambo ambalo
liliwashangaza wafungwa wengi na kushindwa kuamini kumuona Mkuu wa Mkoa ambaye
ni mwakilishi wa Mh. Rais Magufuli katika Mkoa wa Rukwa akila chakula hicho.
Pamoja nae
waliokula chakula hicho walikuwa ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Bw. Nixon
Nzunda, Mtendaji mkuu wa watumishi wa mahakama Bw. Emanuela Munda pamoja na
Katibu wa Mkuu wa Mkoa Frank Mateni.
Mkuu wa Mkoa
aliridhishwa na Chakula hicho baada ya kuona maharage sit u yana chumvi na maji
lakini pia yaliweza kuongezewa viungo na mafuta, jambo ambalo alishindwa
kujizuia kuuliza kama chakula hicho kilikuwa imeandaliwa siku hiyo kwakuwa
walijuwa kuwa mkuu wa mkoa huyo atafanya ziara.
“Chakula
mbona kitamu sana, hiki kimeandaliwa hivi kwakuwa mna taarifa kwamba leo
nafanya ziara katika magereza ama ndio kawaida ya kila siku?” Mkuu wa Mkoa
aliuliza.
 |
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen akielekezwa na maafisa wa magereza maeneo ya mashamba yanayomilikiwa na jeshi hilo katika gereza la Mollo. |
Mmoja wa
wafungwa Isaya Mwambe ambae yupo katika gereza hilo kwa muda wa miaka 16, alitoa
ushuhuda kuwa chakula hicho ndicho wanachokula kila siku na kumtoa hofu mkuu wa
mkoa juu ya ubora wa chakula hicho.
Katika
kuliangalia suala la Afya Mkuu wa Mkoa alipeleleza utoaji wa huduma kwa wale
wanaopatwa na magonjwa na kujibiwa kuwa mara kwa mara wafungwa pamoja na
mahabusu hao hufanyiwa uchunguzi wa kiafya na zahanati ya magereza na hali ikiwa
mbaya kwa mgonjwa basi hupelekwa hospitali ya Mkoa kwa uchunguzi Zaidi.
 |
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen kulia, katibu tawala. Nixon Nzunda kati kati na Emanuel Munda Mtendaji Mkuu wa watumishi wa mahakama wakila chakula kilichoandaliwa kwa wafungwa. |
Kabla ya
kutoa nafasi ya kusikiliza kilio cha mmoja mmoja Mkuu wa Mkoa alisomewa risala iliyobainisha
malalmiko pamoja na changamoto wanazokumbana nazo katika kuruka viunzi ili kuweza
kufikia haki zao.
Mingoni mwa changamoto
walizoziwasilishwa kwa Mkuu wa Mkoa kupitia risala hiyo iliyosomwa na Oswald
Usambo, wafungwa hao walilalamikia mahakama kuweka masharti magumu kwaajili ya
kupatiwa dhamana, kucheleweshwa kupelekwa mahakamani pamoja na kuchelwa kwa
upelelezi.
Lakini
wafungwa hao hawakusita kumshukuru na kumpongeza Mkuu wa Mkoa kwa Kutenga muda
wake na kuweza kufika katika magereza hayo ili kuweza kusikiliza vilio vyao.
“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa tunatoa shukrani zetu za dhati kabisa kwa kuweza
kufika kwetu na kusikiliza kilio chetu, ni Imani yetu kuwa ujio wako ni kama
Musa kwa wana wa Izraeli na kutokana na historia yako tunaamini utatusaidia.”
Baada ya
kusikiliza risala hiyo Mkuu wa Mkoa alitoa nafasi kwa Wafungwa 10 ili kuelezea
kero na manung’uniko yao ambayo risala hiyo haikuyagusia, nafasi ambazo
wafungwa hao walizitumia vilivyo a kuweza kutoa machozi yao.
Mongoni mwa
Wafungwa waliopata bahati hiyo ni Edes Kamanda ambae alifurahia ujio wa Mkuu wa
Mkoa katika gereza na alielezea ujio huo ni alama ya kutatuliwa matatizo yao,
lakini kilio chake kilikuwa ni kuachiwa na kukamatwa tena hapohapo mahakamani
na wenzie wanane jambo ambalo hawakulielewa mpaka anapata nafasi ya kuongea na
Mkuu wa Mkoa.
 |
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen akielekezwa na maafisa wa magereza maeneo ya mashamba yanayomilikiwa na jeshi hilo katika gereza la Mollo. |
|
Mfungwa
Mwingine aliyekaa katika gereza hilo kwa miaka sita Adam Abdallah alitoa
ushauri kwa serikali ili kuweza kuondoa msongamano hawana budi kutoa adhabu
ambazo zitamalizikia vituoni kama vil kwa walevi kuchapwa bakora na kuhoji kuwa
kwa wale wanaume waliowatelekeza wake zao, kuwepo kwenye mahabusu hakusaidii
bali warudishwe kwa wake zao.
Katika
kuhakikisha kila sauti ya Mfungwa inasikika Mkuu wa Mkoa alimuamuru kamanda wa
gereza hilo awape karatasi kila mfungwa ili aweze kuandika yale aliyoyaona
hakufanyiwa haki katika kesi zao zinazoendelea.
“Nataka
kuwahakikishia kwamba hayo mliyoyaelezea kwenye risala, na wale waliopata
nafasi ya kujieleza, na yale ambayo hatujayasikia, yote tunayafahamu, tumekuja
kuwasikiliza shida na kila mtu aeleze kero yake, Lakini mueleze ukweli, uwongo
hautamfikisha mtu popote.” Mkuu wa Mkoa alifafanua.
Pia Mkuu wa
Mkoa aliendeleza kuwakumbusha kuwa Tanzania ni nchi nchi inayoendeshwa kwa
misingi ya sheria na haitakiwi suala hili liwekwe mchagoni, na hapendi kuona
mrundikano katika magereza hayo.
“Hamkuniita,
nimeamua kuja mwenyewe kwakuwa natambua wajibu wangu na pia nafuata maagizo ya
Mh. Rais John Pombe Magufuli, na Nimekuja na timu yangu ambayo sina wasiwasi
nayo, hivyo kuweni watulivu na wavumilivu” Mkuu wa Mkoa alisisitiza.
Lakini
katika kuhakikisha mazingira yanatunzwa Mkuu wa Mkoa alishauri gereza hilo
kutafuta nishati mbadala kwaajili ya kupikia kama vile kinyesi cha ng’ombe
kuliko kutumia kuni ambazo zinapatikana kwa kukata miti.
Baada ya
kuona tofauti ya umri katika gereza hilo, Mkuu wa Mkoa aliamua kuwainua vijana
21 wa chini ya umri wa miaka 18 ili kujua makosa yao na kuweza kuanza
kuyafuatilia.
Katika
safari yake hiyo ya gereza la Mahabusu la Sumbawanga Mkuu wa Mkoa hakuwasahau
wanawake waliokuwa wamefungwa katika gereza hilo, ambapo aliweza kupata nafasi
ya kuona sehemu wanazolala na miundo mbinu mingine na hatimae kutumia muda wa
dakika 55 kusikiliza kero na changamoto za wafungwa hao.
 |
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen akielekezwa na maafisa wa magereza mifugo inayomilikiwa na jeshi hilo katika gereza la Mollo. |
|
Pia Mkuu wa
Mkoa alitoa nafasi 14 kwa wafungwa hao ambapo mmoja wa wafungwa hao Magreth
Musa aliishauri serikali kuweza kuwapa vifungo vya nje wale wenye vifungo vya
chini ya miezi sita ili kuepusha msongamano katika gereza hilo.
Mkuu wa Mkoa
aliwatoa wasiwasi na kuwasihi kuwa wasione kuwa wametengwa isipokuwa serikali
yao inawakumbuka na kuyashughulikia matatizo yao.
“Msijione
kuwa sio watanzania, kumbukeni kuwa tunawajali na kero zenu tutazifuatilia.”
Mkuu wa Mkoa alimalizia.
Gereza La Kilimo la Mollo
Mkuu wa Mkoa
aliweza kufika katika gereza la kilimo la Mollo na kuweza kuangalia miundombinu
kama sehemu za kulalia na jiko la kupikia lakini pia aliangalia vyanzo vya
maji.
Kabla ya
kuweza kutoa nafasi kwa wafungwa kueleza kero zao, Mkuu wa mkoa aliweza
kusomewa risala iliyotawaliwa na kukwama wa rufaa pamoja, kuosekana kwa umeme
na kutumia umeme wa jua na kushindwa
kuelewa utendaji kazi wa bodi ya “parole”.
Baada ya
risala msomaji Datus Uleti aliweza kumshukuru mkuu wa mkoa kwa ziara yake na
kumuomba iwe ni kawaida yake kufanya hivyo, lakini pia hakusita kumuombea mkuu
wa Mkoa afya njema.
“Tunashuru
kwa ujio wako, hatuna cha kukulipa ila tunakuombea afya njema katika utendaji
wako wa azi” Msomaji risala alimaliza.
Mkuu wa Mkoa
alitoa nafasi tano kwa wafungwa hao ambapo miongoni mwa waliotoa kilio ni Michael
Mika aliyemuomba Mkuu wa Mkoa kuwasaidia kupata madawa kwaaijili ya wagonjwa
mbalimbali.
Mkuu wa Mkoa
pia alitoa nafasi kwa wafungwa hawa kupewa karatasi na kila mmoja kuweza
kuandika kero yake na kuwasisitiza kuwa yote watakayoandika yawe ya kweli na
kuwa uwongo hauna faida kwa yeyote.
“Msifikie
kuwa tunafurahia mkijaa, tunapenda magereza yawe matupu lakini haiepukiki maana
kuna wale wa sikio la kufa halisikii dawa lakini pia hatupendi kuona mpo
kizani, mpo hapa ili kuona mwanga na sio kuongezewa kiza.”
Mkuu wa Mkoa
katika kuyaweka mambo sawa alitoa nafasi kwa timu aliyoongozana nayo kuweza
kuzungumza yale yenye majibu ya hapo hapo, ambapo Mkuu wa gereza Jairo
Mwamgunda alisema kuwa wengi wa wafungwa hao hawafikii vigezo vya kupewa parole
n ahata wale wenye sifa, ndugu wa wafungwa hao hawako tayari kuwapokea ndugu
zao napia wale waliofanyiwa makosa hawataki kutoa msamaha.